Sunday, 15 September 2013

FLOYD MAYWEATHER AENDELEZA REKODI YAKE YA KUTOPOTEZA PAMBANO.

BONDIA FLOYD MAYWEATHER{USA},ALFAJIRI YA LEO AMEENDELEZA REKODI YAKE YA  KUTOPOTEZA PAMBANO,BAADA YA KUFIKISHA PAMBANO LA 46,ALFAJIRI YA  LEO,AKIENDELEA KUWA MSHINDI BAADA YA KUMPIGA KWA POINT BONDIA CANELO ALVAREZ{MEXICO},PAMBANO LILILOKUWA GUMU SANA KATI YA MAPAMBANO TAKRIBANI YOTE AMBAYO BONDIA FLOYD MAYWEATHER AMEKUTANA NAYO,
MAYWEATHER AKISINDIKIZWA NA SWAHIBA WAKE MWANA HIPHOP LIL WAYNE, ALIINGIA KWA MBWEMBWE ZOTE,NA ATIMAYE MWISHO BONDIA HUYO ALIFANIKIWA KUIBUKA KIDEDEA BAADA YA WAAMUZI WAWILI KUMPA POINTI ZA JUU ZILIZOPELEKEA USHINDI KWAKE,MWAMUZI WA KWANZA POINTI{116-112},NA WA PILI ALIMPA{117-111}, WAKATI MWAMUZI WA MWISHO PEKEE ALITOA MATOKEO YA SARE YA{114-114}.
FLOYD MAYWEATHER AKIINGIA UKUMBINI HUKU AKISINDIKIZWA NA RAPPER LIL WAYNE PEMBENI.
KWA REKODI ZINAVYOSEMA BONDIA CANELO ALVAREZ{MEXICO}HAKUWAHI KUPOTEZA PAMBANO LOLOTE TOKA AANZE KUPIGANA,AMESHACHEZA MAPAMBANO ZAIDI YA AROBAINI NA  AMESHINDA YOTE ,HIVYO HILI NDILO PAMBANO LAKE LA KWANZA KUSHINDWA,WAKATI MPINZANI WAKE FLOYD MAYWEATHER BADO ANAENDELEZA REKODI YAKE YA KUTOPOTEZA PAMBANO.



No comments: