Sunday, 6 July 2014

Daraja laua na kujeruhi katika mji yanapofanyika mashindano ya Kombe la Dunia{Brazil}

Watu wawili wanaripotiwa kufa na 22 wamejeruhiwa baada ya daraja linalopita juu ya barabara kuvunjika katika mji wa Belo Horizonte ambako baadhi ya mechi za kombe la dunia zinafanyika.
Daraja hilo limeripotiwa kuvunjika Alhamisi ya wiki iliyopita na kuvunja sehemu ya basi huku gari lingine likiwa limenaswa ndani.
Wajenzi wa daraja hilo walipaswa kuwa wamemaliza ujenzi kabla mashindano ya Kombe la Dunia kuanza.
Mji wa Belo Horizonte umesha-host mechi 5 za kombe la dunia hadi sasa na ambapo mechi nyingine ya nusu fainali inatarajiwa kufanyika.

No comments: