Tuesday, 8 July 2014

KAMA KAWAIDA RIHANNA{RIRI}AENDELEA KUWACHANGANYA,BAADA YA DRAKE SASA AJIWEKA KWA BIG SEAN.

Rihanna na Big Sean ni wapenzi! Chris Brown adaiwa kuachana na Karrueche Tran 

Picha:-Big Sean & Rihanna.
Kuna tetesi kuwa Rihanna ambaye kwa muda mrefu kidogo amekuwa single baada ya kuachana na Drake amempata mpenzi mpya, rapper Big Sean.
Kwa mujibu wa mtandao maarufu wa udaku ‘MediaTakeout’, Rihanna na Big Sean walionekana Jumamosi (July 5) wakiwa katika pool party Ya mchezaji wa NBA, Kevin Durant huko Los Angeles.
Mashuhuda walioeleza  kuwa na uhakika walidai kuwa wasanii hao walifika katika eneo hilo kwa pamoja na walikaa na kuishi dakika zote kama couple.
Drake"Dreezy" & Rihanna"Riri"
Tetesi hizi zinaanza kuaminika na baadhi ya watu kwa kuwa hata Big Sean alishaachana na mpenzi wake Nay Rivera kwa hiyo wote hawana kikwazo cha kuwa wapenzi.
Wakati Rihanna akiripotiwa kuanza maisha mapya ya mapenzi na Big Sean (kama ripoti ya media takeout itakuwa kweli), Chris Brown yeye anaripotiwa kuachana tena na Karrueche Tran ambaye huwa na maisha ya kuachana na kurudiana mara kwa mara.
Karrueche & Chris Brown.
Tetesi za kuachana kwa Chris na Karrueche zilichochewa na post ya Karrueche na baadae kila mmoja akafuta baadhi ya picha za mwenzake kama sio zote kwenye mitandao ya kijamii.
“Love what you have before life teaches you to love what you lost.” Aliandika Karrueche Tran kwenye Instagram.
Picha moja ya Birthday alizowahi kusherehekea Chris Brown akiwa na Karrueche Tran.



 

No comments: