Sunday, 6 July 2014

KIPA WA TIMU YA TAIFA YA MAREKANI TIM HOWARD APATA WAKATI MGUMU KWENYE MAPOKEZI NCHINI HUMO.

Tim Howard
Mlinda mlango wa klabu ya Everton ya nchini Uingereza pamoja na timu ya taifa ya Marekani (USA) Tim Howard, amepata wakati mgumu wakati alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Los Angeles akiwa sambamba na kikosi cha The Yanks ambacho kilikuwa nchini Brazil kikishiriki fainali za kombe la dunia za mwaka huu.
Tim Howard, ambaye ameibuka shujaa wa taifa la Marekani kufuatia uwezo mkubwa aliouonyesha wakati wa The Yanks ikicheza michezo ya fainali za kombe la dunia huko nchini Brazil, alipata changamoto hiyo kufuatia kila shabiki aliyekutana naye uwanjani hapo kutaka kumsalimia na kumkumbatia.
Mashabiki wengine walionekana wakimpiga picha kwa ajili ya kumbukumbu zao binafsi, hali ambayo bado ilionekana kumkera lakini alijitahidi kutimiza shauku za mashabiki hao.
Hata hivyo Tim Haward alipewa tahadhari na raisi wa Marekani Barack Obama kwa kumueleza hali halisi iliyokuwepo nchini humo mara baada ya ujasiri aliouonyesha wakati wa mchezo wa hatua ya 16, ambapo USA walipambana na Ubelgiji na kufungwa mabao mawili kwa moja.

No comments: