Saturday, 30 August 2014

DIAMOND APAGAWISHA GERMANY-UKUMBI WAWA MDOGO WATU WAJAA KUPINDUKIA.

Diamond akifanya yake kwenye show yake ya juzi nchini Ujerumani.
MSANII DIAMOND PLATNUMZ{TZ}AMEFANYA SHOW YA KUFURU NCHINI UJERUMANI JUZI BAADA YA KUUJAZA MPAKA KUPITILIZA UKUMBI,HUKU AKIKONGA VILIVYO NYOYO ZA MASHABIKI WAKE WALIOHUDHURIA ONYESHO LAKE HILO,
KUFUATIA KUJAA HADI KUPITILIZA KWA WAPENZI WA BURUDANI KWENYE SHOW HIYO DIAMOND AMEANDIKA MANENO HAYA KUPITIA UKURASA WAKE WA FACEBOOK.... "Haya ndio madhara ya ndugu zetu Mapromoter wa nje kutotaka kuamini na kukubali kuwa mziki wa East Africa sasa umekuwa... mwisho wa siku wanaandaa show kwenye venue ndogo halaf watu wanajaa hadi wanakosa pa kusimama na kuwabidi wapande kwa stage walau wapate pa kupumua..."Alisisitiza Diamond Platnumz.

No comments: