Kwa mujibu Wa documentary ya kituo cha television cha Aljazeera, meno ya tembo yalisafirishwa ndani ya Presidential Diplomatic Bag wakati Wa ziara ya rais Wa China nchini Tanzania. Documentary hiyo inataja "the highest office in the country" kuhusika na biashara haramu ya meno ya tembo. Wanatoa takwimu kuwa 2005 kulikuwa na jumla ya tembo 142,000 nchini, idadi ambayo imepungua kufikia tembo 55,000 tu hasi sasa!
Report implicates China in elephant poaching
Inadaiwa kuwa wanunuzi, raia wa Uchina walinunua maelfu ya kilo za pembe za ndovu nchini Tanzania na kuzitorosha kutoka nchini humo katika ndege ya kibinafsi ya rais wa Uchina Xi Jinping,wakati alipozuru bara la Afrika.Kulingana na shirika la ujasusi la mazingira lililo na makao yake mjini London. Pembe hizo zilinunuliwa wiki moja tu kabla ya ziara ya rais huyo wa Uchina kwenda nchini Tanzania mwaka ulioipita ambapo zilifichwa katika mifuko ya wanadiplomasia ili kutokamatwa. Shirika hilo pia linadai kwamba wajumbe waliokuwa wakiandamana na Rais Xi walinunua viwango vikubwa vya pembe hizo. Uuzaji wa Pembe za ndovu ulipigwa marufuku mwaka 1989 ili kuwazuia wawindaji haramu kuwaua ndovu.

No comments:
Post a Comment