Tuesday, 12 May 2015

Alichosema Ngassa baada ya kumwaga wino Free State Stars ya Afrika kusini leo..

KIUNGO mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Mrisho Khalfan Ngassa ‘Anko’ amesaini mkataba wa miaka minne wa kuitumikia klabu ya  Free State Stars ya Afrika kusini.
Mtandao wa michezo wa Bin Zubeiry umeripoti kuwa Ngassa amesaini mkataba huo leo nchini Afrika kusini baada ya kufikia makubaliano.
“Sasa najiandaa kwa maisha mapya baada ya kucheza Tanzania kwa muda mrefu, hii ni changamoto mpya kwangu, mpira wa Afrika Kusini upo juu sana ukilinganisha na pale kwetu (Tanzania). Nataka kutumia fursa hii kuitangaza soka ya Tanzania, ili klabu zisijifikirie tena kusajili wachezaji wa Tanzania,”Ngassa amekaririwa na Bin Zubiery leo asubuhi nchini Afrika kusini baada ya kusaini mkataba wa miaka 4 kuichezea timu ya Free State inayoshika nafasi ya 9 katika ligi kuu nchini humo.
Kwa upande wake, Kocha Mkuu wa timu hiyo maarufu kama Ea Lla Koto, Mmalawi Kinnah Phiri amesema kwamba amekuwa akimpenda Ngassa kwa muda mrefu na kukutana naye FS ni kutimia kwa ndoto zake za kufanya kazi na kijana huyo siku moja.

No comments: