Sunday, 30 August 2015

RAIS KIKWETE AZINDUA KAMPENI YA MAMA ONGEA NA MWANAO

Mama Ongea na mwanao ni kampeni ambayo imeanzishwa na baadhi ya wasanii wakiongozwa na Steve Nyerere na Wema Sepetu kwa lengo moja tu la kuwaamasisha wazazi kuongea na watoto wao na kuwapa Elimu juu ya mambo mbalimbali kuhusu uchaguzi pamoja kuwahamasisha kuipigia kura CCM chama ambacho wanaamini kinao uwezo wakuwaletea maendelea wayatakayo...
Hafla hiyo ilifanyika Hyatt Regency Kilimanjaro jijini Dar es salaam na mgeni rasmi alikuwa Mh. Jakaya Mrisho Kikwete rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania.
Msanii wa Filamu, Wema Sepetu akimkabidhi Rais Dkt. Jakaya Kikwete tuzo maalum kwa kutambua mchango wake katika kulinda na kuthamini kazi za wasanii nchini ambapo katika kipindi chake cha uongozi wamepata manufaa makubwa. Wema alikabidhi tuzo hiyo kwa niaba ya baadhi wasanii wa filamu na muziki nchini wanaoshiriki katika kampeni ya 'Mama Ongea na Mwanao' yenye lengo la kuwahimiza wanawake kuwahimiza watu kuipigia kura CCM kwa kuwachagua wagombea wake katika uchaguzi mkuu mwaka huu.

Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt. Jakaya Kikwete akitoa hotuba yake ya ufunguzi wa kampeni hiyo.

Wasanii wa Filamu nchini Wema Sepetu na Steven Nyerere wakimkaribisha Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt. Jakaya Kikwete katika Hoteli ya Hyatta Kempinski jijini Dar es Salaam kuzindua kampeni ya 'Mama Ongea na Mwanao' ili aipigie kura CCM. Kampeni hiyo imeratibiwa na wasanii wa filamu wakiongozwa Wema Sepetu na Steven Nyerere.

Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt. Jakaya Kikwete, Waziri wa Sheria na Katiba ambaye pia ni Katibu wa NEC Siasa na Uhusaino wa Kimataifa, Dkt. Asha-Rose Migiro, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Paul Makonda (kushoto) wakiwa na wenyeji wao Wema Sepetu na Steven Nyerere katika uzinduzi wa kampeni ya 'Mama Ongea na Mwanao' ili aipigie kura CCM. Kampeni hiyo imeratibiwa na wasanii wa filamu jijii Dar es Salaam jana.

Umoja wa akina mama wakimkabidhi zawadi ya tuzo Mama Asha Rose Migiro.
Mh,Rais akiongea jambo na Mama Wema Sepetu.
Mh,Rais J.K.Kikwete katika picha na Mc wa shughuli hiyo Zamaradi Mketema.
Wasanii wa Filamu wanaounda umoja huo wa akina mama katika picha ya pamoja na Mh,Rais.
Wema Sepetu na Mama Kanumba.
Wema Sepetu akihutubia.
Mh,Rais J.K.Kikwete akiangalia tuzo aliyokabidhiwa na wamama.
Wamama wakiserebuka wakati wa hafla hiyo.
Wema Sepetu na Mama yake.

No comments: