Wednesday, 28 October 2015

Lowassa apinga matokeo ya uchaguzi TZ

Mgombea Urais kwa tiketi ya UKAWA,Bw,Edward Ngoyai Lowassa akiongea na wanahari leo mchana.



Mgombea wa urais kupitia tiketi ya chama cha CHADEMA Edward LOwassa amesema kuwa hatokubali matokeo ya uchaguzi wa urais yanayoendelea kutolewa na tume ya uchaguzi nchini Tanzania NEC.

Amesema kuwa ana ushahidi wa kutosha kwamba kuna udanganyifu uliofanyika.
Amesema kuwa kura za chama hicho zimepunguzwa katika vituo vingi vya kupigia kura.
Wanadai kwamba kura zilizohesabiwa katika maeneo tofauti haziambatani na matokeo yaliyotolewa. Lowassa ameongezea kwamba maeneo yote ambayo walipata ushindi yamecheleweshwa huku vikishamiri vitendo vya kukamatwa kwa maajenti wa chama hicho,akidai kuwa ni ishara za kutaka kuiba kura.
Chanzo-BBC SWAHILI

No comments: