TAARIFA ZA KUWASILI MWILI WA MAREHEMU LETICIA NYERERE.
 |
| Marehemu Leticia
Nyerere |
Kuna
uwezekano mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Leticia
Nyerere, aliyefia nchini Marekani utawasili nchini mapema kwa ajili ya
maziko tofauti na ratiba iliyokuwa imepangwa awali.Akizungumza na
waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Msemaji wa familia ya
Mwalimu Nyerere, Rose-Mary Nyerere, alisema Balozi wa Tanzania nchini
Marekani, Wilson Masilingi, kwa kushirikiana na familia hiyo wanafanya jitiahada kuusafrisha mwili huo kuja nchini kabla ya Jumatatu iliyokuwa imepangwa awali.
“Ratiba inaonyesha mwili utawasili nchini Januari 18 kulingana na
taratibu za safari, ila tunajaribu kuangalia njia ya kufupisha muda huo
kwa sababu ni mbali tangu mpendwa wetu Leticia alipotutoka,” aliasema.
Alisema mwili huo baada ya kuwasili nchini utaagwa nyumbani kwa Mwalimu
Nyerere, Msasani, jijini Dar es Salaam na taratibu za kuusafirisha
kwenda kijijini Butiama, mkoani Mara kwa ajili ya maziko zitaendelea.
No comments:
Post a Comment