Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. George Simbachawene (Mb) amemuagiza
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala kumsimamisha kazi mara moja Kaimu Afisa
Biashara wa Manispaa ya Ilala Bw. Dennis. N. Mrema kuanzia leo tarehe
07 Januari, 2016 kwa kosa la kusababisha upotevu wa Mapato ya Serikali
kutokana na urasimu wa kukusudia, mazingira ya rushwa na uzembe katika
utoaji wa leseni za Biashara.
Kutokana na hali hiyo Mhe. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI ameelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kumuondoa kwenye nafasi yake Kaimu Afisa Biashara wa Manispaa ya Ilala na nafasi yake kukaimiwa na mtu mwingine ili kupisha uchunguzi zaidi juu ya tuhuma zilizotolewa dhidi yake.
Kutokana na hali hiyo Mhe. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI ameelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kumuondoa kwenye nafasi yake Kaimu Afisa Biashara wa Manispaa ya Ilala na nafasi yake kukaimiwa na mtu mwingine ili kupisha uchunguzi zaidi juu ya tuhuma zilizotolewa dhidi yake.
No comments:
Post a Comment