Tuesday, 11 February 2014

MITCHELE OBAMA AFUNGUKA JUU YA MATUKIO MFULULIZO YA UVUNJAJI SHERIA KWA JUSTIN BIEBER

Baada ya kuona matukio ambayo amekuwa akiyafanya ya uvunjaji sheria the pop teen sensansion Justine Bieber, mpaka kufikia hatua ya baadhi ya Wamarekani, kupiga kura kutaka Bieber arudishwe kwao Canada. 
 Hatimaye the first lady wa Marekani Michelle Obama afunguka na kutoa ushauri wa bure kwa wazazi wa artist huyo na kusema kama angekuwa ni yeye mzazi wa mtoto huyo basi angejaribu kuwa naye karibu muda wote, na kumshauri kipi kizuri cha kufanya.
‘Kwa sababu ni utoto tu ndio anapitia kwa sasa, watoto wanataka uwepo wa karibu wa wazazi wao, wanataka ushauri kama mzazi wake, bado ni mtoto ningekuweka karibu’ alimalizia mke huyo wa Raisi Barack Obama.

No comments: