Monday, 19 May 2014

MWILI WA ADAM KUAMBIANA WAAGWA RASMI-BUNJU B, DAR

Mwili wa Adam Kuambiana ukiandaliwa tayari kwa kuagwa nyumbani kwake Bunju B jana jioni .
MWILI wa mwongozaji na muigizaji wa filamu maarufu Bongo, Adam .Philipo Kuambiana umeagwa rasmi jana nyumbani kwake Bunju B, Dar ambapo ndugu, jamaa, wanasiasa, marafiki wameshiriki tukio hilo. leo asubuhi mwili utapelekwa Viwanja vya Leaders kuagwa na baadaye kuzikwa katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar.
Waombolezaji wakiwa msibani tayari kuaga mwili. Wa tatu kutoka kulia waliokaa mbele ni mke wa marehemu Janeth Rithe ambaye ni Diwani Kata ya Kunduchi, Dar

Watangazaji Sauda Mwilima (kulia) na Zamaradi Mketema (kati) wakiwa msibani hapo. Kushoto ni msanii Shamsa Ford.

William Mtitu (katikati) akiwa na waombolezaji.

Ibada ya kumuombea marehemu ikiendelea.

Mwili wa marehemu Adam Kuambiana ukitolewa nje ya nyumba kwa ajili ya kuagwa.
Baadhi ya wasanii baada ya kuwasili nyumbani kwa marehenu Bunju B.

Mwili wa marehemu ukiwasili nyumbani Bunju B.



Mwili wa marehemu ukishushwa kutoka kwenye gari Bunju B.

No comments: