![]() |
Anastazia Mukabwa & Rose Muhando. |
Inadaiwa kuwa Mukabwa ni aina ya wasanii wenye uwezo mkubwa wa kuimba na kwamba Rose ameiomba Kamati ya Maandalizi ya uzinduzi wake iwasiliane na msanii huyo mapema kuhakikisha anapatikana siku hiyo. “Wapo waimbaji wengi wa Injili natamani wawepo siku hiyo, lakini ningefurahi sana kama ningempata Anastazia Mukabwa wa Kenya, hivyo tayari nimeiomba Kamati yangu ya Maandalizi ifanye kila linalo wezekana aje, Nyimbo zilizopo katika albamu ya Kamata Pindo la Yesu ni Bwana Niongoze, Wewe Waweza, Usiniache, Nibariki, Muongo, Kwema, Kamata Pindo la Yesu na Facebook inayofanya vizuri zaidi.
Ikumbukwe kuwa Anastazia Mukabwa na Rose Muhando walishawahi kukutana kwenye Albam ya pamoja iliyofanya vizuri sana kwenye ukanda huu wa Africa Ya Mashariki hapo Awali,Albam waliyoipa jina la KIATU KIVUE,huku wimbo wa KIATU KIVUE ukikaa kwenye Chati nyingi za muziki wa Injili Africa ya Mashariki.
No comments:
Post a Comment