Monday, 14 July 2014

SCOLARI AJIUZULU RASMI UMENEJA KWA TIMU YA TAIFA-BRAZIL

Vyombo vya habari nchini Brazil vimeripoti kuwa Meneja wa Timu ya Taifa hilo Luiz Filipe Scolari amejiuzulu rasmi nafasi yake hiyo ya umeneja wa timu ya taifa. Tangazo rasmi linatarajiwa kutolewa baadaye (leo). Scolari ambaye analaumiwa kwa kuisababishia timu hiyo ya Taifa{Brazil}kichapo cha mabao 7-1 na Ujerumani alishasema awali kuwa nafasi yake hiyo itafikiriwa upya na chama cha soka cha Brazil baada ya kumalizika kwa Kombe la Dunia.

No comments: