Tuesday, 11 November 2014

Nuh Mziwanda afunguka tuhuma za yeye kupewa kichapo kizito na Shilole

Shilole & Nuh Mziwanda
MWANAMUZIKI wa Bongo Fleva, Nuh Mziwanda amefunguka kuwa  watu wanaomsema vibaya kuhusu yeye kupewa kichapo na mpenzi wake, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ wanakosea kwani anaamini kufanywa hivyo ni mahaba.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii hivi karibuni, Mziwanda alisema kuna taarifa zimeenea kuwa huwa anapigwa na Shilole pindi anapokosea lakini ukweli si kupigwa ‘livebali ni kupigwa kimahaba.
Shilole"Shishi Beiby" & Nuh Mziwanda.
“Jamani kupigwa wanakozungumzia watu sielewi lakini mimi baby pia ananipiga kimahaba, wanaosema kuwa mpenzi wangu ananipiga washindwe, watuache kwa raha zetu,”alidakia Shilole.

No comments: