Saturday, 17 January 2015

DIAMOND, ALI KIBA WAKUTANA UKUMBINI, WACHUNIANA


Baadhi ya wasanii wa Bongo fleva wakiwa kwenye mkutano. Duh! Kama ulikuwa unaamini kuwa lile bifu la wakali wawili wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Ali Saleh Kiba, limekwisha, basi umenoa baada ya jamaa hao kukutana ukumbini na kuchuniana. Ishu hiyo ilijiri kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Double Tree Hilton jijini Dar, juzikati ambapo wasanii mbalimbali walikutanishwa na kampuni moja ya huduma ya simu za mkononi ili kuzungumza na wanahabari juu ya maandalizi ya tamasha. Waandishi wetu, wakiwa wameingiwa na roho ya kutaka ‘ubuyu’, hatimaye muda wa kuingia Kiba ukawadia ambapo alitinga na timu yake ya watu wanne. lipofika, Kiba alikaa sehemu ya viti vya kushoto akiwa bize na mrembo mmoja wakichati kabla ya Diamond kutimba na timu yake kubwa.

No comments: