Thursday, 26 February 2015

CHID BENZ AHUKUMIWA JELA MIAKA MIWILI AU KULIPA FAINI YA LAKI 9.

Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania Rashidi Abdallah Makwaro Maarufu kama (Chid Benzi) amehukumiwa kifungo cha miaka miwili jela au kulipa faini ya shingili laki tisa baada ya kupatikana na hatia ya makosa matatu ikiwemo kukutwa na dawa za kulevya aina ya heroin yenye thamani ya sh. 38,638, bangi ya sh. 1,720 na vifaa ya kuvutia dawa hizo kijiko na kigae.
Taarifa zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa nguli huyo wa muziki wa Hiphop amefanikiwa kulipa faini hiyo na sasa yuko huru kuendelea na mambo mengine ya kulijenga taifa ikiwemo shughuli zake za kimuziki.

No comments: