Zaidi ya abiria Arobaini wa basi la
kampuni ya Majinja linalofanya safari zake kati ya Mbeya na Dar es
Salaam wamefariki dunia kwenye ajali ya barabarani iliyotokea katika
eneo la Changarawe wilayani Mufindi huku abiria wengine 22 wakijeruhiwa
baada ya basi hilo kugongana uso kwa uso na lori namba T.689 APJ mali ya
kampuni ya Cipex ya Dar es Salaam lililokuwa limebeba kontena.
Mashuhuda wa jali hiyo iliyohusisha basi la majinja lenye namba za
usajiri T438 CDE.lililokuwa linatokea mkoani Mbeya kwenda jijini Dar es
Salaam wameeleza kuwa lori hilo lililokuwa katika mwendo kasi ghafla
liliingia kwenye mashimo makubwa ya barabarani na kupoteza mwelekeo
hivyo kulifuata basi kwenye upande wake na kusababisha ajali hiyo.
Baadhi ya majeruhi walionusurika kwenye ajali hiyo iliyotokea
majira ya saa tatu na dakika 40 wamesema awali walimuonya dereva wa basi
hilo kupunguza mwendo lakini hakuwasikiliza na walipofika katika eneo
la Changarawe kilometa chache kutoka mjini mafinga ndipo walipokumbana
na dhahama hiyo.
| Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Barabarani mkoa wa Iringa, Salim Asas Abri (kulia) akiwa na viongozi wengine wakiwajulia hali manusura wa ajali hiyo. |
ITV imeshuhudia miili ya watu 42 ikishushwa katika hospitali ya
wilaya ya Mufundi huku majeruhi sita waliokuwa katika hali mbaya kati ya
22 wakihamishiwa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Iringa ambapo mkuu wa
mkoa wa Iringa Bibi Amina Masenza amezungumzia ajali hiyo na kusema kuwa
ni moja ya tukio la ajali mbaya ya barabarani kuwahi kutokea katika
mwaka huu.
| Miongoni mwa manusura 22 wa ajali ya basi la Majinja lenye namba za usajili T438 CED wakiwa wamelazwa katika hospitali ya Mkoa Iringa kwa matibabu. Abiria 42 walipoteza maisha katika ajali hiyo. |
Zoezi la uokoaji katika eneo la tukio lilihusisha vyombo karibu
vyote yaani jeshi la zima moto na uokoaji, jeshi la kujenga taifa JKT
kutoka kikosi cha 841 kj.huku uongozi wote wa mkoa wa Iringa
ukikusanyika katika eneo la tukio ambapo baadhi ya wananchi walimzonga
mkuu wa mkoa wa Iringa kulalamikia mashimo hayo ambayo yanaelezwa kuwepo
kwa zaidi ya mwezi mmoja.
MAJINA YALIYOPATIKANA HADI SASA NI:
Baraka Ndone (dereva), Yahya Hassan ( kondakta), Ester Emanuel, Lusekelo Enock, Jeremia Watson, Digna Solomoni, Frank Chiwango, Luteni Sanga, Teresia Kamingage, Dotto Katuga, Ester Fidelis, Paulina Justine, Mbamba Ipyana, Catherine Mwate, Mwajengo, Ndulile Kasambala, Zera Kasambala, Rebeka Kasambala, Shadrack Msigwa, Mathias Justine, Juliana Bukuku, Cristina Lyimo, Martin Haule na Dominick Mashauri, Omega Mwakasege.
Wengine ni Ester Willy, Lucy Mtenga, Erick Shitindi, Edwiga Kamiyeye, Frank Mbaula, Mustapher Ramadhani, Kelvin Odubi, Upendo William, Charles Lusenge, Neto Sanga, Pili Vicent, Daniel, Jacob Doketa Iman Mahenge , Juma Sindu, Dk A. Shitindi, Six Erick, Frank Mbaule,
Wengine waliokuwepo katika ajali hiyo wametambuliwa kwa jina moja Amadi, Musa, Elias, Raphael, Hussein na Oswald.
Basi hilo lilianza safari mjini Mbeya likiwa na abiria 37.
MAJINA YALIYOPATIKANA HADI SASA NI:
Baraka Ndone (dereva), Yahya Hassan ( kondakta), Ester Emanuel, Lusekelo Enock, Jeremia Watson, Digna Solomoni, Frank Chiwango, Luteni Sanga, Teresia Kamingage, Dotto Katuga, Ester Fidelis, Paulina Justine, Mbamba Ipyana, Catherine Mwate, Mwajengo, Ndulile Kasambala, Zera Kasambala, Rebeka Kasambala, Shadrack Msigwa, Mathias Justine, Juliana Bukuku, Cristina Lyimo, Martin Haule na Dominick Mashauri, Omega Mwakasege.
Wengine ni Ester Willy, Lucy Mtenga, Erick Shitindi, Edwiga Kamiyeye, Frank Mbaula, Mustapher Ramadhani, Kelvin Odubi, Upendo William, Charles Lusenge, Neto Sanga, Pili Vicent, Daniel, Jacob Doketa Iman Mahenge , Juma Sindu, Dk A. Shitindi, Six Erick, Frank Mbaule,
Wengine waliokuwepo katika ajali hiyo wametambuliwa kwa jina moja Amadi, Musa, Elias, Raphael, Hussein na Oswald.
Basi hilo lilianza safari mjini Mbeya likiwa na abiria 37.

No comments:
Post a Comment