Leo ninaomba nikushirikishe wimbo huu
mpya ambao umefanywa na vijana 20 ambao wameingia katika hatua nyingine
ya juu zaidi baada ya kuchujwa kutika kundi la vijana zaidi ya 17510
waliojitokeza katika usahili wa KINONDONI TALENT SEARCH 2015 pale coco
beach.. hawa vijana 20 hawa ndio pekee waliopita viwango vyote na
kuonekana ni waimbaji bora ambao wako tayari kwa ajili ya kuchujwa na
hatimaye kumpata mshindi hapo baadae mwezi ujao..wimbo unaitwa KIPAJI
CHAKO AJIRA YAKO ambayo kauli mbiu hii inabeba maana nzima ya dhima na
kusudi la kuanzishwa kwa mashindano haya ikiwa ni kuhakikisha kila
mkazi wa kinondoni ananufaika na kipaji chake alichopewa na
Mungu.nafurahi kwani nina matumaini kwa nafasi yako uliyonayo
utaifanikisha nyimbo hii kuwafikia wasikilizaji wote Tanzania kwani hata
hivyo ujumbe ulioko katika wimbo huu unawahusu vijana wote
Tanzania walioo na ndoto zao mtaani kupitia vipaji vyao.. ila wamekata
tama hawajui wapi waanzie.. vijana wenzao wameona wawape moyo kwa wimbo
huu maalumu..
NAKUOMBA KWA NAFASI YAKO NISAIDIE KUUFIKISHA WIMBO HUU KATIKA MASIKIO YA WASIKILIZAJI WAKO WALIO WENGI.
Jina la wimbo – KIPAJI CHAKO AJIRA YAKONAKUOMBA KWA NAFASI YAKO NISAIDIE KUUFIKISHA WIMBO HUU KATIKA MASIKIO YA WASIKILIZAJI WAKO WALIO WENGI.
Mtunzi/composer – PETER MSECHU
Mpangilio wa mziki/music director – PETER MSECHU
Studio live recording – REAL STUDIO
Producer – MASANJA

No comments:
Post a Comment