Monday, 6 July 2015

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu yawahukumu Mramba na Yona kwenda jela miaka 3.

Kushoto Gray Mgonja{Shati la Draft},Daniel Yona{katikati}na Basil Mramba.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewahukumu kwenda jela miaka mitatu waliowahi kuwa mawaziri ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao ni Basil Mramba aliyekuwa waziri wa Fedha na Daniel Yona aliyekuwa waziri wa Nishati na Madini kwa matumizi mabaya ya madaraka kuisababishia serikali hasara ya shilingi bilioni 11.7

Hata hivyo aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha,Gray Mgonja ameachiwa huru baada ya kukutwa hana hatia.

Chanzo Itv na Radio One.

No comments: