Wednesday, 19 August 2015

Mtoto wa miaka miwili achomewa ndani ya nyumba kisa wivu wa mapenzi

Mtoto wa miaka 2 Wilayani Makete, achomewa ndani ya nyumba kisa wivu wa mapenzi.

-Yadaiwa Mama wa mtoto alituhumiwa kutembea na mume wa mtu.


Mtoto wa miaka miwili Joshua Sepi wilaya ya Makete amefariki dunia baada ya nyumba aliyokuwa amelala kuchomwa moto.

Chanzo cha mauaji hayo ni wivu wa mapenzi ambapo mtuhumiwa (aliyechoma nyumba) alimtuhumu mama wa mtoto huyo kuwa anatembea na mume wake.

Kamanda Mutafungwa amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.

No comments: