Thursday, 10 September 2015

PICHA:-YALIYOJIRI WAKATI ASKOFU JOSEPHAT GWAJIMA AKIONGEA NA WANAHABARI KWENYE HOTELI YA LAND MARK JUZI.

Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Bishop Josephath Gwajima (katikati) akizungumza kwenye mkutano na Wanahabari katika Hoteli ya Land Mark. 

ASKOFU wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima leo amefunguka kuhusu tuhuma zilizotolewa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrosia na Maendeleo (Chadema) Dkt. Willbrod Slaa na kusema kiongozi huyo ni muongo, akidai madai yote dhidi yake hayana ukweli wowote. Akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari na baadhi ya waumini na wachungaji wake kwenye Hoteli ya LandMark jijini Dar es Salaam, alisema amelazimika kuweka mambo wazi kwa kuwa kiongozi huyo kushindwa kuwa mkweli. Alisema chanzo cha Dkt. Slaa kuondoka Chadema si ujio wa Edward Lowassa kujiunga na chama hicho, bali aliyesababisha ni mkewe aliyemtaja kwa jina la Josephine.
….Gwajima akionesha hisia zake.
Wanahabari wakichukua matukio.
Wanahabari wakiwa katika mkutano huo sambamba na waumini wa kanisa hilo.
Wafuasi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima la Gwajima wakiwa katika mkutano wa wanahabari uliofanyika katika Hoteli ya Land Mark Ubungo jijini Dar.
Mkutano ukiendelea.
Mmoja wa wananchi aliyejitambulisha kwa jina la Hebron Mwakanjara akiondoka ukumbini hapo baada ya kuuliza swali na kujibiwa asivyotarajia na kuzomewa na wafuasi wa Gwajima.
…akiondoka Hotelini hapo.
Wafuasi wa kanisa la Ufufuo na Uzima lake Bishop Josephat Gwajima wakishangilia mara baada ya kuondoka hotelini hapo.

No comments: