Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania, Mh. Jakaya Mrisho Kikwete mwishoni mwa wiki amefungua kiwanda kikubwa zaidi kuliko kingine chochote katika Afriaka Mashariki, kinachozalisha saruji ambacho kinamilikiwa na kampuni ya Dangote Group ya Nigeria inayomilikiwa na tajiri mkubwa barani Afrika Alhaji Alio Dangote.
Uzinduzi huo umefanyika kwenye kiwanda hicho kipya kilichopo eneo la Msijute, Mtwara Vijijini mkoa wa Mtwara na kuhudhuriwa na wafanyabiashara 170 kutoka Nigeria ambao wamehudhuria sherehe hiyo kama wageni wa Alhaj Dangote.
![]() |
Picha inayokionyesha Kiwanda hicho. |
Kiwanda hicho kipya pia kinatarajia kuajiri watu 1500 katika ajira za moja kwa moja na watu 9000 watapata ajira zisizokuwa za moja kwa moja. Kiwanda hicho kitazalisha tani za ujazo milioni tatu kwa mwaka kimegharimu dola za kimarekani milioni 600, ikiwa ni uwekezaji mkubwa zaidi kutoka nje kuingizwa katika uchumi wa Tanzania.
No comments:
Post a Comment