![]() |
| Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira, |
Miongoni mwa walioanguka hadi jana wakati matokeo ya uchaguzi huo yakiendelea kutangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) ni Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira, ambaye melipoteza Jimbo la Bunda, mkoani Mara.
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Anne Kilango Malecela, amekwama kutetea jimbo lake la Same Mashariki, mkoani Kilimanjaro.
Mwingine aliyepoteza ubunge ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Uwezeshaji na Uwekezaji), Christopher Chiza, katika Jimbo la Buyungu, mkoani Kigoma.
![]() |
| Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Uwezeshaji na Uwekezaji), Christopher Chiza |
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Aggrey Mwanri, ameanguka na kulipoteza jimbo la Siha, mkoani Kilimanjaro.
![]() |
| Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Aggrey Mwanri |
DK. Kebwe Stephen Kebwe, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, ameangushwa katika Jimbo la Serengeti, mkoani Mara, baada ya kupata kura 39,232 dhidi ya 40,059 za mpinzani wake, Marwa Ryoba wa Chadema.
![]() |
| DK. Kebwe Stephen Kebwe, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii |




No comments:
Post a Comment