Ni siku ambayo tayari historia imeandikwa kwenye vichwa vya Habari za Siasa Tanzania ambapo Dk. John Pombe Joseph Magufuli ametangazwa kuwa mshindi wa kiti cha Urais kwenye Uchaguzi mkuu uliofanyika October 25 2015.
Rais JK na Dk. Magufuli ndani ya Ikulu baada ya matokeo ya Urais kutangazwa October 29 2015 Kwa maana hiyo Dk. Magufuli anakuwa Rais anayekuja kubadili nafasi ya Rais Jakaya Kikwete na kuwa Rais wa awamu ya tano Tanzania, Dk. Magufuli amealikwa Ikulu Dar es Salaam Tanzania na Rais Kikwete na kupongezwa kwa ushindi huo muda mfupi tu baada ya kutangazwa kupitia TV waliyokua wakitazama pamoja.
Dk. John Magufuli akipokea pongezi za mgombea urais wa ACT Anna Mgwira.
Rais JK, Mama Salma Kikwete kwa pamoja wakimpongeza Dk. John Magufuli.








No comments:
Post a Comment