SHIRIKA
la Viwango Tanzania (TBS), limeamuru shehena ya mafuta ya petroli
iliyoagizwa kutoka Falme za Kiarabu irejeshwe ilikotoka kutokana na
kubaini hayana ubora unaotakiwa kwa matumizi ya magari na mitambo.Akitoa
taarifa hiyo Dar es Salam jana, Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo, Joseph
Masikitiko alisema, vipimo vya maabara vya sampuli ya mafuta hayo
vimeonesha kuwa hayafai kwa matumizi.Alisema hayo
ni matokeo ya ukaguzi wa hivi karibuni wa shehena hiyo yenye ujazo wa
tani za metriki 38,521.018 katika meli ya MT. Ridgebury John B,
yaliyokuwa yasambazwe na kuuzwa nchini.
Alisema, "Vipimo vinaonesha kuwa baadhi ya matakwa ya viwango vya mafuta ya petroli hayajafikiwa, hivyo kuamuru yarejeshwe yalikotoka. Kiwango cha ubora cha mafuta ya petroli ni TZS 672:2012/ EAS 158:2012 ambacho hakikufikiwa".
Matakwa ya kiwango ambacho mafuta hayo hayakukidhi ni pamoja na kuwa na kemikali zilizo na oksijeni ndani yake ambazo husababisha madhara kwenye injini za magari na mitambo.
Alisema, "Kiwango cha petroli hakiruhusu uwepo wa kemikali hizo kwenye mafuta hayo kwa sababu zinaua injini, kuhatarisha afya za watu na kuharibu mazingira kutokana na kusababisha moshi mchafu mwingi".
Alisema, "Vipimo vinaonesha kuwa baadhi ya matakwa ya viwango vya mafuta ya petroli hayajafikiwa, hivyo kuamuru yarejeshwe yalikotoka. Kiwango cha ubora cha mafuta ya petroli ni TZS 672:2012/ EAS 158:2012 ambacho hakikufikiwa".
Matakwa ya kiwango ambacho mafuta hayo hayakukidhi ni pamoja na kuwa na kemikali zilizo na oksijeni ndani yake ambazo husababisha madhara kwenye injini za magari na mitambo.
Alisema, "Kiwango cha petroli hakiruhusu uwepo wa kemikali hizo kwenye mafuta hayo kwa sababu zinaua injini, kuhatarisha afya za watu na kuharibu mazingira kutokana na kusababisha moshi mchafu mwingi".
No comments:
Post a Comment