Tuesday, 9 February 2016

Makamishna wawili wa ZEC wasema hawatambui uamuzi wa kufuta matokeo.

Makamishina wawili kati ya saba wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) leo wamesema hawatambui uamuzi wa kufuta matokeo ya uchaguzi Zanzibar.
Wamesema uchaguzi wa marudio ni batili.


katika taarifa ya habari (ITV) ,wamejitokeza kamishna na kuzidi kuusema ukweli kuwa mambo ya jecha hayana uhusiano na ZEC ni yake binafsi na yasichukuliwe ndio msimaamo wa ZEC.

Wakizidi kumruka Jecha kama CCM walivyoanzaa kumkimbia Jecha ,makamishna wamedai kuwa hawajui wapi Jecha anapokeaa maagizo na malalamiko kibao yaliyowakilishwa na CCM yalitupiliwa mbali hata jechaa alishiriki katika msimamo wa kuyakataa maombi ya CCM ambayo Tume ilikuwa hayawahusu ni mambo ambayo yalitakiwa kupelekwa mahakamani ,jecha alitoweka na kutoa misimamo akiwa hajulikani alipo .

kwa kweli CCM hawana pa kujificha , eti na wao hawakupendelea kutangazwa uchaaguzi kurudiwa kwa kuwa walikuwa wamekwisha shinda ,suaali walijuaje kama walikwisha shinda ? Mbona hawadai kumtaka Jecha aendelee kutangaza matangazo ,
Source-ITV 

No comments: