Friday, 1 April 2016

Kamishna Mkuu wa zamani TRA Mahakamani na wengine Wawili.

Mwaka 2012-2013 Serikali ya Tanzania ilikopa Dola za kimarekani  milioni 600 ‘trilioni 1.3’ kutoka benki ya Standard ya Uingereza kwa ajili ya miradi mbalimbali ya Maendeleo kwa makubaliano ya kulipa deni hilo pamoja na riba ya 1.4% inasemekana katika mazingira yasiyojulikana fedha iliongezwa na kuwa  2.4%.
Kwa taarifa ya Serikali iliyotolewa na aliyekuwa katibu Mkuu Ombeni Sefue siku kadhaa zilizopita alieleza kuwa katika mkopo huo hawakuhitaji wakala lakini mwaka 2013 iligundulika kuwa fedha Taslimu Dola milioni 6 ziliingizwa katika akaunti ya kampuni ya Egma ambayo mwenyekiti wake ni aliyekuwa Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania ‘TRA’ Harry Kitilya.
April 01 2016 Harry Kitilya, Sioi Solomoni na aliyekuwa afisa mwandamizi wa benki ya Stanibic tawi la Tanzania, Shose Sinare wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es salaam kwa tuhuma mbalimbali zikiwemo za kula njama kutenda kosa pamoja na kosa  la kughushi na kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.
Wakili wa Serikali upande wa Mashitaka Oswald Tibabyekomya ametoa maelezo kuwa……>>>’kosa ambalo linawagusa pamoja ni kughushi nyaraka ambao ni mkataba wa makubaliano unaoonesha kwamba Stanibic Bank iliingia makubaliano na kampuni ya Egma kwa ajili ya kutafuta mkopo kwa ajili ya Serikali, mkataba ambao ulikuwa wa uongo, kiasi cha fedha kilichohusika kwenye kosa la kujipatia fedha kwa udanganyifu ni dola za kimarekani milioni 6′
Kutokana na makosa yanayowakabili, watuhumiwa wamenyimwa dhamani na kesi yao itasomwa tena April 8 2016.


TAKUKURU yawafikisha mahakamani Kamishna Mkuu Mstaafu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitilya (kati) sambamba na Waliokuwa Wafanyakazi wa Benki ya StanBic Tanzania, Sioi Sumari (kushoto) na Shose Sinare (kulia), wakiwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,
Makosa walio shitakiwa nayo ni kugushi na kutakatisha fedha kiasi cha USD 6 ML
 


No comments: