Friday, 20 May 2016

Diamond, Tiwa Savage, Mafikizolo na Cassper Nyovest kuonekana kwenye kipindi kipya cha E! Entertainment ya Marekani


Diamond, Tiwa Savage, Mafikizolo na Cassper Nyovest kuonekana kwenye kipindi kipya cha E! Entertainment ya Marekani
Kituo cha runinga cha Marekani, E! Entertainment kimetangaza ujio wa kipindi kipya ‘E! VIP’ kitachokuwa kinaonyesha maisha ya mastaa wa Afrika.
Diamond Platnumz, Tiwa Savage, D banj, Mafikizolo na Cassper Nyovest ni moja ya mastaa wa mwanzo wa Afrika ambao wataanza kuonekana kwenye kipindi icho kinachoanza tarehe 12 mwezi wa juni.
Taarifa hiyo ilitolewa na Mkurugenzi mtendaji na masoko wa kituo icho, Colin McLeod siku ya jana ambapo alisema wameamua kuzindua kipindi hicho kipya kutokana na mafanikio makubwa ya kipindi cha E! News Special. “E! is committed to bringing audiences across the continent more original, local content and we areproud to showcase some of Africa’s biggest names in music and entertainment in this new series.” Colin McLeod alielezea.
Pia waliwatangaza Dolapo na MzzAbby kuwa ndiyo watangazaji wa kipindi hicho.

No comments: