LICHA ya kukana kuwa hakufika kwenye pati ya sherehe ya kuzaliwa ya mama yake Wema, Mariam Sepetu iliyofanyika katika ukumbi wa Samaki Samaki, Masaki jijini Dar es Salaam juzikati, inadaiwa kuwa Idris Sultan, mtangazaji wa Kituo cha Redio cha Choice FM, ambaye ni mpenzi wa sasa wa muigizaji nyota Wema Sepetu, alizuiwa getini kuingia ndani ya ukumbi, kisa na mkasa, Ijumaa lina kila kitu.
![]() |
| Wema Sepetu. |
![]() |
| Mama Wema |
“Idris wa watu ambaye alikuwa akijiandaa kupaki gari akawa hana jinsi, akageuza na kuondoka,” kilidai chanzo hicho.
Ikazidi kudaiwa kuwa, hata baada ya pati Wema hakwenda kule hotelini kuonana na Idris kama alivyosema, badala yake yeye, Mkongo na kampani yao walielekea Maisha Club ambako walikula bata hadi kuchwee.



No comments:
Post a Comment