| Msanii wa Kimataifa kutoka nchini Marekani Neyo amewasili jijini Mwanza
jioni hii akitokea Dar es Salaam na kupokelewa na umati mkubwa wa wakazi
wa jiji hilo kama Mfalme katika Uwanja wa Ndege wa jijini Mwanza.
Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania ndio wadhamini wakuu wa
Jembeka Festival 2016 kwa kushirikiana na Shirika la Ndege la Fastjet,
SYSCORP Cooperation, CF Hospitals, KK Security, Samsung, EF Outdoor,
Lacairo Hotel, Ndege Insurance, Jembe Media Group pamoja na Coca Cola.
Msanii huyo anatarajiwa kutumbuiza katika tamasha hilo kwa kupiga ‘Live
Music’ katika uwanja wa CCM Kirumba ambapo msanii wa kimataifa kutoka
nchini, Diamond Platnumz, FID Q, Stamina, Mr. Blue, Ney wa Mitego, Maua
Sama, Rubby, Baraka Da Prince, Juma Nature, MO Music na wengine wengi
watapanda jukwaa moja na msanii Neyo. |
No comments:
Post a Comment