Wednesday, 19 March 2014

ATHARI ZA MGOMO WA DALADALA MANISPAA YA MORO

MADEREVA wote wa daladala Manispaa ya Morogoro leo wamegoma kutoa huduma ya usafiri wakilalamikia kukamatwa hovyo na maafande wa Kikosi cha Usalama Barabarani katika manispaa hiyo.
Akizungumza na tovuti hii, mmoja wa madereva wa daladala hizo, Bw. Ramadhani Shukuru alisema kwamba kwa siku gari linakamatwa mara mbili na kwamba ukifikishwa kituoni unalipishwa faini ya shilingi 90,000/=
"Unakamatwa asubuhi unalipa 90,000/= makosa matatu, ukiachiwa na kuanza kazi ukifika Kihonda unakamatwa tena ukijitetea askari anakwambiaa yeye hausiki na kukamatwa kwako kwani amekukamata kwa makosa mengine unaenda tena kituoni wanakukamua 90,000/= nyingine kesho unakamatwa tena, sasa si bora tuegeshe magari tukalime matombo!" alisema Rama.
KUTOKANA NA MGOMO HUO,WANAFUNZI IMEBIDI KUTUMIA USAFIRI WA MALORI KUWAHI SHULENI.



Wanafunzi wa shule mbalimbali za Manispaa ya Morogoro wakiwa kwenye lori baada ya mgomo wa madereva daladala leo.
Wanafunzi wa shule mbalimbali za Manispaa ya Morogoro wakisubiri usafiri wa kwenda shule bila mafanikio katika kituo cha mabasi kilichopo Mkoani Morogoro.

No comments: