Tuzo ya mwalimu bora zaidi duniani imezinduliwa rasmi.
Tuzo hiyo yenye thamani ya dola milioni moja,
itakabidhiwa kwa mwalimu ambaye anafanya kazi ya ualimu na ambaye
atathibitisha kuwa mchango wake kwa jamii umekuwa bora zaidi kuliko
walimu wengine wote duniani.Pesa hizo zitatolewa kwa kipindi cha miaka kumi, lakini mwalimu huyo ataendelea kufundisha angalau kwa miaka mingine 5.
Tuzo hiyo ambayo imezinduliwa na kupewa baraka zote na Varkey Gems, shirika ambalo hutoa mchango mkubwa katika sekta ya elimu duniani,Shirika hili linaungwa mkono na mtawala wa Dubai, Sheikh Mohammed bin Rashid al Maktoum.
Mwenyekiti wa tuzo hiyo ni Rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton. Bwana Clinton amesema kuwa ni muhimu sana kuwavutia watu bora zaidi kuwa walimu na pia kuwaza kuwathamini na kuthamini kazi zao.
Je,Unadhani mwalimu wako anaweza kushinda tuzo hii?
No comments:
Post a Comment