Thursday, 8 May 2014

Dkt,REGINALD MENGI ADAI RUSHWA NI KIKWAZO KATIKA KUKUZA UCHUMI WA AFRICA YA MASHARIKI.

Juhudi za kukuza uchumi Afrika Mashariki hazitafanikiwa iwapo rushwa haitadhibitiwa-Dk.Reginald Mengi
Mwenyekiti wa  mfuko  wa   sekta binafsi  nchini   Dk. Regnald mengi  amesema itakuwa vigumu kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kukuza uchumi kama hazitadhibiti tatizo sugu la rushwa  linaloendelea kujikita katika sekta mbalimbali
Dr.Mengi ameyasema hayo jijini arusha katika hafla ya utiaji saini mkataba wa   msaada   wa   euro milioni 2.3 zilizotolewa na jumuiya ya ulaya kwa ajili ya kuimarisha ulinzi katika ukanda  wa bahari ya hindi.
Dk.Mengi ambaye  pia ni mwenyekiti mtendaji wa makampuni ya ipp amesema  tatizo la rushwa  limeendelea kushika kasi  na  udhibiti wake unaendelea kuwa mgumu kutokana na utaratibu unaotumika kulishughulikia  ambao umejikita zaidi kwa wanaotoa  kwa watu wadogo.
Kwa upande wake mwenekiti  wa baraza  la wafanyabiashara  afrika  mashariki  Bw. Felexs  Mosha  na  mwenyekiti  wa watendaji  wakuu   wa  makampuni   nchini   bw  ally  mafuruku   wamesema  pia  nchi za     wanachama  wa  jumuiya  hiyo   zinakabiliwa  na   tatizo  la  gharama  kubwa  za  uwekezaji  na  ukosefu  wa  taarifa  muhimu  

Naye  naibu  katibu mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeshughulikia fedha na utawala Jean Cloude  amesema  msaada  huo  wa  jumuiya ya  ulaya  utasaidia  kuimarisha  ulinzi  hasa  eneo  la  bahari  ya  hindi .
 Balozi wa umoja wa Ulaya hapa nchini  Bw.Filiberto  Sebregondi  pamoja  na  kuelezea  azma  ya  jumuiya  ya  ulaya  ya  kuendelea  kuisadia  jumuiya  ya  afrika  mashariki  amesema  pamoja  na  changamoto  zinazojitokeza    zikishughulikiwa   upo  uwezekano mkubwa  wa  kufikiwa  kwa  malengo   tarajiwa
Msaada  huo   wa   euro milioni 2.3  kutoka jumuiya  ya  ulaya   (eu) ni  mwendelezo  wa  kampeni  za  jumuiya  hiyo  kuisadia  jumuiya  ya  afrika  mashariki    ,ambapo kwa kipindi cha mwaka 2010 kiasi cha euro mili 37.5  zimetolewa

No comments: