Thursday, 29 May 2014

IBADA YA KUMBUKUMBU YA MWAKA MMOJA TOKA KIFO CHA MSANII A.MANGWAIR.

Padri Octaviani Msimbe akiongoza ibada ya kumbukumbi ya kifo cha Albart Mangweha nyumbani kwao Kihonda 'Mazimbu Road' Morogoro

FAMILIA ya msanii nyota wa muziki wa Bongofleva marehemu Albert Keneth Mangweha aliyefariki ghafla  nchini Afrika Kusini May 28 mwaka jana, Siku ya jana, may 28 familia hiyo iliifanya ibada nje ya viwanja vya nyumba yao iliyopo Kihonda 'Mazimbu Road' mkoani Morogoro,ikiwa ni Ibada ya kumbukumbu ya mwaka mmoja toka kifo cha mpendwa wao huyo aliyekuwa na nyota ya kupendwa na  wengi.
Katika lbada hiyo iliyoongozwa na Paroko wa kanisa la Mtakatifu Monica Kihonda Padri Octaviani Msimbe ilihudhuliwa na wasanii pamoja na mchumba wa marehmu Mangweha  Michelle Louise.
mchumba wa marehmu Mangweha  Michelle Louise.
 


Kwa mujibu wa msemaji wa familia hiyo mama mzazi wa msanii huyo Bi,Denisia Mangweha, baada ya kukamilika kwa lbada hiyo jana jioni katika ukumbi wa Samaki Samaki Kihonda kulifanyika shughuri nyingine ya kumkumbuka msanii huyo.
Mama Mangweha akipokea sakrameti takatifu
 
Mama Mangwea akitoa shukrani kwa watu walioshiriki lbada hiyo.
 
" Pale Samaki samaki kutakuwa na shughuri mbili, ya kwanza itaanza saa 12 jioni hadi saa mbili usiku na mafariki wa marehemu watafanya shughuri yao kuanza saa 2 usiku hadi majogoo hivyo tunawakaribisha wote mliofika kwenye ibada hii na mungu awabariki kwa kunikimbilia toka kifo cha mwanangu,mapaka hii leo sina cha kuwalipa mungu atawalipa asanteni sana"alisema mama huyo mwenye uso wa upole.
Msanii wa bongofleva Mgaza Pembe' M-2 THE- P ambaye alikuwa na marehemu Mangweha Afrika Kusini akipiga picha za matukio ya lbada hiyo,
 

No comments: