Msanii
Jacob Steven ‘JB’ amedondoka katika Viwanja vya Leaders wakati
akimuelezea msanii mwenzake marehemu Adam Kuambiana.
Tukio hilo limetokea wakati wa zoezi la kuaga mwili wa marehemu kabla ya maziko yatakayofanyika baadaye makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam. Marehemu Kuambiana alifariki dunia ghafla Jumamosi ya Mei 17 mwaka huu wakati akipelekwa katika Hospitali ya Mama Ngoma iliyopo Mwenge, Dar.
Tukio hilo limetokea wakati wa zoezi la kuaga mwili wa marehemu kabla ya maziko yatakayofanyika baadaye makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam. Marehemu Kuambiana alifariki dunia ghafla Jumamosi ya Mei 17 mwaka huu wakati akipelekwa katika Hospitali ya Mama Ngoma iliyopo Mwenge, Dar.
Star huyo mkubwa wa filamu nchini Jacob Stephen(JB) ambaye hivi majuzi alienda nchini Uturuki kwa ajili ya ziara ya kikazi kwa wiki mbili
amekatisha ziara yake hiyo na kurudi nchini kuja kumzika msanii mwenzake
Adam Kuambiana aliyefariki juzi. JB tayari alishafanya kazi kadhaa na
Kuambiana kwani hata filamu yake mpya
iliyotoka wiki kadhaa nyuma inayoitwa Hukumu Ya Ndoa Yangu imeongozwa na
Adam Kuambiana. Kupitia mtandao mmoja wa kijamii jana JB aliandika
"Tumefanikiwa kupata nafasi moja tu ya kurudi Dar es salaam kwa ajili ya
msiba .ahsanteni wenzangu kwa kukubali niwawakilishe, mbaki salama
nawapenda.". Kuambiana anazikwa leo Jumanne . Katika safari ya Uturuki ambayo imedhaminiwa na Princess Casino JB aliongozana na Wasanii wenzake Ray, Irene Uwoya na King Majuto.



No comments:
Post a Comment