Tuesday, 27 May 2014

MSANII RACHEL HAULE WA BONGO MOVIE AFARIKI DUNIA!

Msanii wa Bongo Movie, Rachel Haule 'Recho' (pichani), amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es slaaam. Habari zilizotua ndani ya Ngessa blogspot na kuthibitishwa na Mwenyekiti wa Bongo Movie, Bw,Steve Nyerere, zimesema kuwa Recho alikwenda Muhimbili jana kujifungua ambapo mara baada ya kujifungua mtoto alifariki na yeye hali yake kuwa mbaya, ilibidi ahamishiwe ICU ambako hali ilizidi kuwa mbaya na baadae kufariki dunia.
Kifo cha Recho kimekuja ndani ya wiki moja baada ya kufariki kwa msanii mwingine wa Bongo Movie Marehemu Adam Kuambiana Jumamosi iliyopita, kifo hiki kimeleta mshituko mkubwa kwenye tasnia ya  filamu za kibongo. Habari na picha zaidi zitawajia baadae.
Baadhi ya wasanii wa Bongo Movies wakiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili baada ya taarifa za msiba wa msanii mwenzao, Rachel Haule 'Recho' mapema leo.

Mume wa marehemu Recho, George Saguda,akiwa na simanzi nzito kufuatia kifo cha mkewe.

 

No comments: