May 28 kupitia You heard ya XXL Clouds FM ilikuwa ni stori kuhusu
uhusiano wa Kimapenzi kati ya Msami {Dansa}wa THT na mwigizaji toka Bongo Movie Irene Uwoya, katika siku ya
jana alisikika Msami akikanusha uhusiano huo, lakini mpenzi wake
Rehema aliweka wazi kuwa ni kweli Msami ana uhusiano wa kimapenzi na
Irene Uwoya.
Siku ya May 29 2014 alitafutwa Irene Uwoya na
kuulizwa na Soudy Brown kama ni kweli ana uhusiano wa kimapenzi na Msami
na swali la kwanza lilitaka kujua uhusiano wao umekuepo toka lini?
Mahojiano yalikuwa kama hivi:-
Irene Uwoya: ‘Siku nyingi’
Soudy Brown: Msami kama namuona, unampa huduma zote?
Irene Uwoya: ‘Sanaaa kila kitu’
Soudy Brown: Uhusiano wenu utadumu au ndio kama wa Ndikumana?
Irene Uwoya: ‘Yakudumu kwa sababu nampenda’.
Soudy brown alimpa Irene taarifa kuwa mpenzi wa zamani wa Msami
amekasirika kwa sababu Irene kaingilia mapenzi yao jibu kutoka kwa Irene
likawa ‘hiyo haijalishi kwa sababu nampenda’

No comments:
Post a Comment