Saturday, 16 August 2014

RAIS JACOB ZUMA AMTEUA BINTI YAKE MWENYE MIAKA 25 KUSHIKA WADHIFA WA JUU SERIKALINI

Thuthukile Zuma

Thuthukile Zuma amehamishwa kutoka katika nafasi ya afisa uhusiano wa umma (Public Liaison officer) na kupandishwa cheo ndani ya miezi miwili akiwekwa katika nafasi muhimu na yenye nguvu " Mkuu wa wafanyakazi" katika wizara ya huduma za posta na mawasiliano Raisi wa africa ya kusini Jacob Zuma ameshutumiwa kwa kuwa na mfumo wa upendeleo (Nepotism) baada ya kumteua mtoto wake wa kike mwenye umri wa miaka 25 kushikilia cheo kikubwa serikalini.
Rais Jacob Zuma
Thuthukile ni mtoto wa mwisho katika watoto wanne wa Zuma, ambaye alipokea degree ya heshima ya Anthropology na kukabidhiwa cheo hicho mwezi wa tano mwaka huu baada ya baba yake (Raisi Zuma) baada ya kuchagua baraza lake la mawaziri. nafasi hiyo aliyopewa ambayo inasemekana kutokutangazwa kabla, itakuwa ikimuingizia paundi 55,764 karibu randi milioni moja ambayo ni sawa na shilingi 154,631,365.14 kwa mwaka

No comments: