Friday, 31 October 2014

VANESSA MDEE; HIZI NDIO SIRI USIZOZIJUA KUHUSIANA NA VANESSA MDEE

Vanessa Mdee{Vee Money}

Akiwa anahojiwa na jarida moja la huko nchini Kenya Vanessa Mdee, afunguka mengi ambayo hajawahi kuyasema sehemu nyingine yeyote ile, na kwa wengi wanaomfahamu mkali huyu wa anayezidi ku-make headlines na single yake ya “hawajui”, watabaki midomo wazi kwa vile ambavyo walikuwa hawavijui kabisa kuhusu mwanamuziki huyu kutoka Tzee.
Moja ya mambo ambayo vanessa huwa hafanyi kabisa mbali na kuwa mwanamuziki, mtangazaji na mwanaharakati ni kupika, Vanessa alifunguka na kusema hata akiwa nyumbani kwake ishu nzima ya kupika haimjii akilini kabisa. Tofauti na wanawake wengi wa afrika, hii ishu ni moja kati ya vitu vilivyotokea kuwashangaza wapenzi wengi na wadau wanao mzimia Vanessa.
Vanessa Mdee
Siku alipotoa hit single yake ya “hawajui”, Hii ni moja ya single aliyoitoa kwa watu ambao walikuwa hawamkubali hasa baada ya maneno yao kuzidi kusema kuwa Vanessa hakustahili tuzo ya Kilimanjaro Music Awards aliyoipokea na wengine kusema hakuwa teyari kupokea tuzo hiyo, jambo hili lilimhuzunisha sana Vanessa, hii ilimsukuma vanessa kuandika kuhusu watu wale ambao walikuwa hawamkubali(Haters), na kutoa kitu hiki kinachozidi ku-make headlines kila siku,

No comments: