Tuesday, 4 August 2015

NUH NA SHILOLE WAENDELEA KUIGIZA KWENYE MAPENZI YAO.

Nuh na Shilole.
Kupitia sakata la kumtongoza aliyekuwa Miss{Tz}2006 Wema Sepetu na atimaye kurekodiwa sauti
Nuh mziwanda  amesema kuwa  sauti inayosikika kwenye audio hiyo iliyovuja akisikika akimtongoza wema sio yake, amedai hiyo audio imetengenezwa.
"“Hili suala nalichukulia kawaida na naona ni ushamba na upu*vu ha hawana akili hata kidogo. Kama ni kweli angemfuata shishi akamwamba kwamba ‘mpenzi wako kafanya kitu Fulani Fulani kwangu’ sio kutangaza. Na kama kweli, kwanini asingesema wengine wanaomtongoza na akaweka mitandaoni? Ni wema na watu wake wote ndio wamefanya hivi! Siku ya kwanza shishi alilipokea vibaya  lakini baada ya kumuelewesha kanielewa.” Nuh alisema
Baada ya kuzimia kwa mshtuko wakati taarifa hizi zikimfikia na atimaye hali yake kuwa salama.
Shilole amefunguka kuwa hana ugomvi na mtu na wala hajali kama wametengeneza au vipi kwasababu Nuh alishamuomba msamaha na wamesameheana.
Akiongea na mtandao wa Bongo5 Nuh amemshutumu Wema na timu yake kwa kuamua kumchafua yeye na mpenzi wake shilole ambaye tayari wamepatana.

No comments: