Saturday, 7 March 2015

MATONYA NA TUNDAMAN WAPATANA.

Kwenye Bongo Fleva ishu ya Tunda Man na Matonya kutokuwa na maelewano mazuri ni moja ya News zilizosikika sana, kila mmoja alikuwa akilalamika tofauti kuhusu mwenzake, jana March 6 mastaa hao walikutana kwa pamoja ndani ya studio za Clouds FM, wakati wa show ya Leo Tena.
Tunda Man amesema anachohisi alimkosea Matonya ni kusema kwamba alimtungia nyimbo lakini  hataki tena kuzungumzia ishu hiyo, amesema leo itakuwa mara ya mwisho kuzungumzia jambo hilo na kuomba radhi kwa yote yaliyotokea, hana tatizo lolote na Matonya.
Matonya amesema kuwa Tunda Man ni mdogo wake ambaye wamekutana vizuri na walikuwa wanaishi vizuri lakini alipata wasiwasi baada ya kuona kila siku kuna maneno yanaibuka ambayo hakupendezwa nayo, yeye binafsi anampenda Tunda Man na hata familia yake, kwa nafasi yake kama kaka ameamua kumsamehe.
Tunda amesema hawakuwahi kuonana tangu mwaka 2007.. Matonya akamalizia kwamba kwa sasa wako tayari kwa pamoja kuingia studio kufanya collabo.
Kusikiliza story yote ya Hekaheka bonyeza play hapa chini…

No comments: