![]() |
| Pam Daffa. |
Pam D: Kama kuanza sijaanza leo lakini rasmi nimeanza mwaka jana na ngoma yangu ya Nimempata ambayo nimeshirikiana na Mesen Selekta.
Mwandishi: Kwa mara ya kwanza kabisa wewe kuanza kuimba ulianza na wimbo upi?
Pam D: Niliimba wimbo ambao nilikuwa nimeshirikiana na Darasa kupitia Studio za Classic Sound chini ya Mona Gangstar lakini kipindi chote hicho sikuwa siriazi na wala sikujua watu wananichukuliaje lakini sasa hivi nimekuja rasmi.
Mwandishi: Wengi wanasema kwamba Mesen anakuinua sana kwenye muziki wako kuanzia kwenye utunzi wa mistari mpaka kukuandalia, ikoje hiyo?
Pam D: Ifahamike tu kwamba hata kama Mesen ni ndugu yangu lakini familia yetu sisi karibu wote ni wanamuziki na kwenye kazi kila mtu anafanya yake, mimi naandika mwenyewe na yeye ni prodyuza.

No comments:
Post a Comment