Tuesday, 25 August 2015

MASHA ASHTAKIWA RASMI LEO JIJINI DAR ES SALAAM.

Waziri wa Zamani wa mambo ya Ndani Mh. Laurance Masha
Aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani na Mwanachama wa CHADEMA, Lawrence Masha jana alikamatwa na Jeshi la Polisi, leo amefikishwa Mahakama ya Kisutu Jijini Dar

-Anashtakiwa kwa kosa la kuzuia Polisi wasitimize majukumu yao(Obstructrion of Justice)


Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani Laurence Masha amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam mchana huu baada ya kushikiliwa jana alipofika kituo cha polisi Oysterbay kutoa dhamana kwa baadhi ya wanafunzi waliokamatwa kwa kosa la mkusanyiko usiokuwa na kibali.

Mbele ya Hakimu mkazi kisutu Emilius mchauri, wanafunzi hao 19 wamesomewa shtaka la kukusanyika kwa lengo la kutaka kuandamana bila kibali .Watuhumiwa hao wamekana shtaka na dhamana yao iko wazi .

Kwa upande wa Bw.LAURENCE MASHA shtaka lake ndilo linasomwa wakati huu ingawa kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoa wa kipolisi Kinondoni anatuhumiwa kwa kosa la kutumia lugha ya matusi kituo cha polisi .Pamoja na kuzuia Polisi kutimiza majukumu yake{Obstruction of Justice} Watuhumiwa wote wa chadema wanatetewa na wakili PETER KIBATALA.

No comments: