![]() |
| Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini, Jenerali Davis Mwamunyange, |
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Rais Kikwete alisema kuwa katika miaka 10 ya uongozi wake, amefanya mambo mengi kwa Watanzania pamoja na kuliacha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) likiwa katika hali nzuri ya kiutendaji.
Alisema hakuna nchi inayoweza kupata maendeleo mbalimbali kama haina jeshi imara kutokana na kuwapo vitendea kazi vya kutosha na madhubuti vinavyoimarisha jeshi hilo.
Jenerali Mwamunyange alisema katika kipindi chote cha uongozi wa Rais Kikwete, ameimarisha JWTZ na kutimiza mahitaji ya jeshi hilo.
Alisema pamoja na changamoto ndogo zilizobaki, lakini anaamini serikali ijayo itazifanyia kazi na kuendeleza pale alipoishia ili kuwa na jeshi imara.

No comments:
Post a Comment