UKAWA WAFUNGUA KESI MAHAKAMA KUU KUDAI UHALALI WA SHERIA YA KULINDA KURA MITA MIA MBILI.
 |
| Wakili Peter Kibatara. |
CHADEMA
imefungua shauri Mahakama Kuu ya Tanzania, ikitaka tafsiri sahihi ya
sheria kama mpiga kura anaruhusiwa kukaa mita 200 kusubiri matokeo
yatangazwe.
-Kesi hiyo imefunguliwa chini ya hati ya haraka sana.
Kulinda kura: Wakili Peter Kibatala afungua kesi Mahakama Kuu
Tayari wakili jembe na nguli Peter Kibatala akiambatana na wanasheria
nguli wa Ukawa Prof Safari, Mallya na Tundu Lissu asubuhi ya leo
amefungua kesi mahakama kuu kuishitaki NEC kwa ukiukwaji wa sheria juu
ya wananchi kukaa mita mia mbili na kulinda kura.
Kesi imefunguliwa under certificate of urgency nadhani kama sijakosea
kwa kiswahili ni 'hati ya dharura' ili isikilizwe na tafsiri itoke kabla
ya uchaguzi.Tayari jalada lishapelekwa kwa pilato na wanasheria nguli
wa Ukawa wamejipanga kwa hoja za nguvu na ushahidi wa kutosha.
Pia jopo la wanasheria nguli wa UKAWA wameiomba mahakama kuu ya Tanzania
kutoa tafsiri ya kisheria juu ya matamshi ya rais wa nchi kuwa alitumia
mamlaka gani kuvaa kazi za tume.
Leo,16th
October 2015, tumefungua Kesi chini ya hati ya haraka sana (certificate
of extreme urgency) shauri nambari 37 la mwaka 2015 katika Mahakama Kuu
ya Tanzania (Main Registry) tukiomba Mahakama Kuu itoe tafsiri sahihi
ya kifungu cha 104 (1) cha Sheria ya Uchaguzi Tanzania na itamke iwapo
wapiga kura na watu wengine wenye shauku wanaruhusiwa au la kukaa KWA
UTULIVU umbali unaozidi meter 200 kutoka kituo cha kupigia kura/kufanya
majumuisho ya kura.
Tumeiomba pia Mahakama Kuu itamke iwapo ni halali kwa Rais wa nchi kutoa
matamko aliyoyatoa kwa namna ya katazo kwa wapiga kura/raia wenye
shauku kukaa KWA UTULIVU umbali unaozidi meters 200 kutoka kituo cha
kupigia kura/kufanya majumuisho.
Pia tumeiomba Mahakama Kuu itamke iwapo Rais ana mamlaka hayo kisheria kwa kuzingatia Sheria ya Uchaguzi Tanzania.
Tunasubiri taratibu za kiMahakama kuhusu shauri tajwa.
No comments:
Post a Comment