Sunday, 22 November 2015

SAMATTA AFANYIWA BONGE LA SURPRISE NA FAMILIA YAKE!!

Mbwana Samatta akivalishwa taji na mdogowake muda mfupi baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Mwl. Julius Kambarage Nyerere leo asubuhi
Familia ya Mzee Ally Samatta leo ilikuwepo uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa ajili ya kumpokea na kumpongeza mtoto wao Mbwana Samatta kwa mafanio makubwa aliyoyapata kwenye soka kwa kutwaa ubingwa wa Afrika pamoja na kuwa mfungaji bora wa michuano hiyo kwa mwaka huu.
Mbwana Samatta (kulia) akilakiwa na babayake mzazi mzee Ally Samatta
Mzee Ally Samatta ambaye alikuwa ameambatana na familia nzima wakiwemo kaka na wadogo zake Mbwana Samatta amesema, hawajawahi kwenda kumpokea Samatta uwanja wa ndege wakiwa kama familia lakini leo waliamua kufanya kitu cha tofauti kwasababu wanahisi hakuna kitu kingine ambacho wanaweza kukifanya kikamfurahisha zaidi ya kwenda uwanja wa ndege kama familia na kumlaki mtoto wao.
Samatta (katikati) akiwa pamoja na familia nzima iliyokwenda uwanja wa ndege kumpokea

Mara baada ya kutua uwanja wa ndege, Samatta alijikuta akishindwa kujizuia kuonsesha furaha aliyokuwanayo baada ya kukutana na familia yake nzima ikiwa inamsubiri uwanjani hapo kwa ajili ya kumpongeza kwa mafanikio yake pamoja na kusalimiana nae.


Mashabiki na wadau wa soka nao wakaungana na familia hiyo kumpongeza Samatta ambaye alikuwa ameambata na Thomas Ulimwengu kabla ya kuchukuliwa na viongozi wa TFF na kupelekwa sehemu maalumu ambako watapumzika wakisubiri kuingia kambini kuungana na kikosi kizima cha Stars.

No comments: