Dkt,Ali Mohamed Shein |
Kabla ya uamuzi huo, wagonjwa waliopatiwa huduma za vipimo hivyo walikuwa wakilipia kati ya Sh. 100,000 na 150,000 kwa mashine ya CT-Scan na Sh. 100,000 kwa Utra-Sound wakati huduma za X-ray ni Sh. 30,000.
Katibu wa Hospitali ya Mnazi Mmoja, Hassan Makame, alisema huduma bure za afya kwa vipimo, ni utekelezaji wa agizo la Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein.
Alisema uongozi wa hospitali hiyo ulipokea agizo la kufutwa kwa gharama za vipimo kwa wagonjwa Oktoba mosi, mwaka huu.
Alisema chini ya maagizo hayo, wagonjwa wote wametakiwa kufanyiwa uchunguzi wa vipimo bure ili kuwaondolea usumbufu wananchi wasiokuwa na uwezo wa kumudu gharamza za vipimo.
No comments:
Post a Comment