Wakati
Rais John Magufuli akitimiza siku 31 akiwa amejifungia Ikulu kutatua
kero za nchi bila kusafiri nje ya nchi, Rais mstaafu Jakaya Kikwete
(pichani) ameendelea kujumuika katika hafla za kimataifa baada ya
kuonekana nchini Afrika Kusini juzi akiwa mwalikwa wa Mkutano wa China
na Afrika.
Tangu aingie madarakani Novemba 5, Rais Magufuli amepiga marufuku safari za nje kwa watendaji wa serikali bila ya kibali maalumu cha Ikulu.
Alifikia uamuzi huo baada ya kubainisha katika hotuba yake ya ufunguzi wa Bunge la 11 mwezi uliopita kuwa safari za kimataifa zinatafuna mabilioni ya fedha za walipa kodi.
Rais Magufuli hajasafiri kwenda nje ya nchi mbali na kwenda Dodoma kwa ajili ya kumwapisha Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na kuzindua Bunge.
Picha zilizotumwa na Ofisi ya Makamu wa Rais jana, zilimwonyesha JK akiwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, aliyemwakilisha Rais Magufuli kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika na China, uliomalizika jana jijini Johannesburg.
JK ameonekana katika picha hizo akitembelea mabanda ya maonyesho ya mkutano huo ulioandaliwa na China ili kujadili mikakati ya ushirikiano baina yake na Afrika.
Tangu aingie madarakani Novemba 5, Rais Magufuli amepiga marufuku safari za nje kwa watendaji wa serikali bila ya kibali maalumu cha Ikulu.
Alifikia uamuzi huo baada ya kubainisha katika hotuba yake ya ufunguzi wa Bunge la 11 mwezi uliopita kuwa safari za kimataifa zinatafuna mabilioni ya fedha za walipa kodi.
Rais Magufuli hajasafiri kwenda nje ya nchi mbali na kwenda Dodoma kwa ajili ya kumwapisha Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na kuzindua Bunge.
Picha zilizotumwa na Ofisi ya Makamu wa Rais jana, zilimwonyesha JK akiwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, aliyemwakilisha Rais Magufuli kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika na China, uliomalizika jana jijini Johannesburg.
JK ameonekana katika picha hizo akitembelea mabanda ya maonyesho ya mkutano huo ulioandaliwa na China ili kujadili mikakati ya ushirikiano baina yake na Afrika.

No comments:
Post a Comment